.
19th December, 2018
Chama cha Kutetea Maslahi ya Walimu nchini, KNUT, kimetoa ilani ya mgomo wa walimu kaunzia Januari tarehe mbili mwaka ujao, ili kulalamikia kile kinachodaiwa kuwa udhalimu na unyanyasaji wa tume ya TSC dhidi ya walimu. Katibu mkuu wa KNUT, Wilson Sossion, hasa ameitaka tume ya kuwaajiri walimu, TSC, kubatilisha uhamisho wa walimu zaidi ya elfu tatu, kwa misingi kwamba uhamisho huo ulifanywa kinyume cha taratibu na sera za tsc kuhusu uajiri na uhamisho wa walimu.