17th December, 2018
Kurunzi ya mpango wa serikali kupokea bunduki haramu kutoka kwa umma leo hii umeangazia mojawapo ya mitaa sugu zaidi hapa jijini Nairobi maeneo ya Eastlands. Ilani ya siku 90 iliyotolewa na serikali tayari imeanza kutekelezwa na waendesha mpango huo wanasema kuwa wataangazia kwa kina maeneo ya mitaa ya mabanda ambako kwa muda mrefu wahalifu sugu wamekuwa wakitamba.