13th December, 2018
Kwa mara ya kwanza tangua salamu za heri Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga kwa pamoja wamezuru eneo la Nyanza ili kuzindua miradi mbalimbali ukiwemo ule mpango wa Huduma ya Afya kwa wote. Katika hotuba zao wamesisitiza umuhimu wa utangamano nchini. Wengine waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na Naibu Rais William Ruto na viongozi kutoka eneo hilo.