13th December, 2018
Kizaazaa kilishuhudiwa katika makaburi ya Wanyororo mjini Bahati baada ya jamaa za mwendazake kukosa kusikizana iwapo wamzike marehemu aliyeaga dunia wiki jana au la. Mkewe marehemu na binamuze wawili walijirusha ndani ya kaburi na kukatalia huko wakati mahubiri yalipokuwa yakiendelea.