10th December, 2018
Kinara wa ODM Raila Odinga amewasuta wanasiasa kutoka mkoa wa Bonde la Ufa wanaopinga vita vinavyoendelea dhidi ufisadi wakikisia kudhulumiwa kikabila. Raila aliyezungumza katika kanisa la PCEA kiangonya katika kaunti ya Kiambu? amesema vita hivi vitaendelea, na kuwa yeye na rais uhuru kenyatta hawatosita kwenye juhudi zao kupambana na jinamizi hili.