.
5th December, 2018
Rais Uhuru Kenyatta amesema hatatia saini mswada wa nyongeza ya mishahara ya wabunge kwani utakuwa mzigo mkubwa kwa wananchi. Aidha amesema yeye anaunga mkono wananchi kuwa kile taifa linalohitaji zaidi ni utoaji wa huduma na sio nyongeza ya mishahara. Rais alikuwa akizungumza alipohudhuria hafla ya kufuzu kwa vijana walioasi uraibu wa dawa za kulevya na unywaji pombe katika kituo cha mama care kaunti ya Kiambu.Takriban vijana sabini waliobadili tabia walifuzu.