.
3rd December, 2018
Familia moja mtaani Bahati mjini Nakuru imepoteza watoto watatu hapo jana jioni. Baada ya kugongwa na gari katika eneo la Maili tisa. Inaarifiwa kwamba dereva wa gari hilo hakusimama licha ya kusababisha maafa. Watoto hao ni Brian Nderitu, mwenye umri wa miaka kumi na mitano, aliyekuwa akisubiri kujiunga na elimu ya sekondari baada ya kupata alama mia tatu tisini na moja katika mtihani wa KCPE, Ruth Wanjiru mwenye umri wa miaka kumi na mitatu, pamoja na mdogo wao, Anthony Njenga mwenye umri wa miaka sita.