26th November, 2018
Familia moja kutoka eneo la Kapkuis eneo Bunge la Soy Kaunti ya Uasin Gishu inaomboleza kifo cha mtoto wao ambaye aliuawa baada ya makundi mawili ya vijana, moja linaloshikilia imani ya tohara ya kitamaduni na ile ya imani ya tohara ya kisasa kukosana. Marehemu Mathew Kipruto alipgwa rungu kichwani na kufariki kwenye zogo hilo.