.
21st November, 2018
Matumaini ya Gavana wa Wajir Mohammed Abdi Mohamud kuendelea kusalia mamlakani sasa yamo mikononi mwa jopo la majaji sita wa mahakama ya upeo ambao wamekuwa wakisikiza kesi inayoharamisha shahada yake. Gavana huyo aliamua kufika katika mahakama hiyo ya juu baada ya mahakama kuu na ile ya rufaa kufutilia mbali kuchaguliwa kwake kwa misingi kwamba hana vyeti halali.