.
20th November, 2018
Jamii ya wamaasai wanaoishi katika eneo lililopo karibu na mbuga ya wanyama ya amboseli ilifanya uchaguzi wa viongozi wao. Uchaguzi huo ulifanywa ili kupata watakaosimamia shughuli za shamba hilo pana. Shamba hilo ni asilimia tisini ya Mbuga ya Amboseli na hivyo jamii huona haja ya usimamizi thabiti wa rasilmali hiyo ambayo ni sehemu ya mapato ya nchi kupitia utalii. Kwenye uchaguzi huo hata watoto wachanga walihesabiwa kama sehemu ya kura zilizopigwa na ilivyo kawaida kwenye uchaguzi wowote ule, wizi wa kura ni suala ambalo liliibuka.