20th November, 2018
Inspekta Generali wa polisi Joseph Boinnet amewaahidi, wasimamizi wa msikiti wa Riyadha ulioko Kaunti ya Lamu, kuwa idara ya polisi itawaunga mkono katika jitihada zao za kuhifadhi msikiti huo,uliotengenezwa mwaka wa elfu moja mia nane tisini na mbili na kuchapishwa rasmi kwenye gazeti la serikali kama turathi ya kitaifa mwezi Aprili mwaka huu. Shirika la UNESCO limeweza kuwapa ufadhili wa utunzaji wa mnara wa msikiti huo, huku viongozi waislamu wa msikiti huu wakitazamia serikali itaweza kuwasaidia katika utunzi wa raslimali hii ya kitaifa. Tarehe ishirini na mbili hadi ishirini na tano msikiti huu utakuwa mwenyeji wa tamaduni za lamu na zile za maulid ambazo hufanyika kila mwaka.