.
17th November, 2018
Viongozi kutoka eneo la Magharibi leo wametofautiana wazi wazi kuhusu mustakabali wa jamii hiyo kisiasa kabla ya uchaguzi wa mwaka 2022. Baadhi wakitaka kuwepo kwa chama kimoja cha jamii ya waluhya nao wengine wakipinga. Mbunge maalum Godfrey Ososi alijipata matatani baada ya kumtetea kinara wa chama cha ODM Raila Odinga.