.
1st November, 2018
Mamia ya wanafunzi wa taasisi ya mafunzo ya kiufundi ya Kipkabus Kaunti ya Uasin Gishu wameandamana wakipinga uhamisho wa mkuu wa taasisi hiyo isaac kwambok huku wakidai kuwapo kwa mwingilio wa kisiasa. Wakiongozwa na Mwenyekiti wao Rugut Kigen,wanafunzi hao wameshikilia kuwa hawatarejea madarasani wala kufanya mitihani yao inayoanza juma lijalo bila kupata hakikisho la kufutiliwa mbali kwa agizo la kumhamishia mkuu huyo hadi Kaunti ya Baringo. Hata hivyo Mkuu wa Idara ya Mafunzo ya Kiufundi kwenye Kaunti ya Uasin Gishu Michael Rugut amesema tayari uhamisho wa mkuu huyo umesitishwa kwa kipindi cha muda usiojulikana. |