.
28th October, 2018
Chama cha wataalam wa dawa za tiba kimejitokeza kuzungumzia mageuzi katika sheria ya afya mwaka 2018 iliyowasilishwa bungeni na kiongozi wa wengi bungeni Aden Duale.
Katika kikao na wanahabari chama hicho kimekumbatia mapendekezo hayo , hususan katika kipengee kinachotaja faini mpya ya shilingi milioni moja kwa wale watakaopatikana wakiuza dawa kwa umma kinyume na sharia katika mapendekezo zaidi, chama hicho sasa kitakuwa na wawakilishi watatu katika halmashauri ya kusimamia dawa za tiba na sumu nchini.