27th October, 2018
Seneta wa Baringo Gideon Moi yuko katika kaunti ya homa bay kwa siku mbili kusaidia kuchangisha fedha za miradi ya wanawake na kanisa la Adventist la Wikondiek. Moi amekaribishwa katika kaunti hiyo na viongozi wa eneo hilo, seneta moses kajwang' mwakilishi wa kike gladys wanga, miongoni mwa viongozi wa serikali ya kaunti hiyo. Kwenye mkutano wa leo, siasa za ni nani rais Kenyatta anapaswa kumkabidhi madaraka zilizuka.