22nd October, 2018
Wadi ishirini katika Kaunti ya Taita Taveta zitafaidika na mpango wa ujenzi wa majosho 75 ya kuwaogesha mifugo katika ufadhili wa serikali ya kaunti. Mpango unasaidia kukomesha magonjwa yanayotokana na kupe. Maeneo hayo yalitengwa kutokana na usimamizi mbaya. Gavana wa kaunti ya taita taveta granton samboja amesema serikali yake inaangazia sana kuimarisha hali ya kilimo. Wakulima eneo hilo wanasema siku zilizopita wamepoteza mifugo kutokana na matumizi ya njia zisizofaa katika kudhibiti magonjwa ya mifugo.