.
20th October, 2018
Mwili wa mwanamme mmoja mwenye umri wa makamu umepatikana ukiwa uchi kando mwa barabara ya Meru?Isiolo.kwa mujibu wa mashahidi haikuwa imedhibitika kiini cha maafa hayo manake mwili huo haukuonyesha dalili za majeraha yoyote. Hata hivyo baadaye ilifichuka kwamba marehemu ni mmoja wa wachuuzi wa vyuma vikuukuu mjini isiolo huku makundi ya wanaorandaranda mitaani wakimtambua kama rafiki yao.mwili huo ulipelekwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya rufaa ya isiolo.