19th October, 2018
Sherehe za maadhimisho ya sikukuu ya Mashujaa itafanyika hapo kesho katika kaunti ya Kakamega ikiwa ndio mara ya kwanza sherehe hizi zinafanyika katika kaunti hiyo. Makundi mbalimbali ya usalama yamekuwa katika uwanja wa bukhungu kwa matayarisho ya hafla hiyo. Gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya amesema hafla hiyo imeipa kaunti ya kakamega hadhi kubwa. Rais kenyatta ataongoza hafla hiyo.