.
17th October, 2018
Ni rasmi sasa kuwa Jaji wa mahakama kuu James Wakiaga amechukua usukani kuendesha kesi ya mauaji inayomkabili mwanahabari Jacque Maribe.
Wiki iliyopita jaji Jessei Lessit alitangaza kuwa kesi hii itaendeshwa na jaji mwingine akikosa kutoa sababu madhubuti kuhusiana na mwelekeo huo. Hata hivyo katika siku yake ya kwanza kuendesha kesi hii, jaji Wakiaga ametimua kivumbi kwa vyombo yvya habari humu nchini akionya wanahabari wanaokikuka kanuni za kuripoti habari za kortini.