16th October, 2018
Waziri wa usalama wa ndani fred matiangi ametangaza kuwa machifu sasa watapewa mafunzo ya kijeshi ili kusaidia katika harakati za kudumisha usalama na kukabiliana na kero la ugaidi. Waziri matiangi alikuwa akizungumza katika mjini nyeri baada ya kufungua rasmi warsha ya siku tatu ya kuwapa mafunzo maafisa wa utawala. Mwanahabari wetu ibrahim karanja ana maelezo zaidi.