.
15th October, 2018
Watoto wawili mapacha wenye umri wa miaka minne wamefariki baada ya nyumba yao kuteketezwa na moto. Wawili hao walikuwa wameachwa na wazazi wao wakiwa peke yao nyumbani wakati mkasa huo ulipotokea. Naibu OCPD wa Nyeri Bernard Amugune alithibitisha kisa hicho na kusema kuwa polisi na idara husika wanafanya uchunguzi kubaini chanzo cha moto huo. Aliwaomba wazazi kuwa waangalifu kila wanapotoka nyumbani na kuacha watoto.