15th October, 2018
Mwenyekiti wa Tume huru ya uchagzui na mipaka nchini IEBC Wafula Chebukati ametoa changamoto kwa tume ya kupambana na ufisadi EACC kuwatia mbaroni wahusika katika sakata ya ufujaji wa pesa za tume hiyo wakati wa uchaguzi mkuu ulipita. Chebukati ambaye alikuwa akizungumza kwenye uzinduzi wa zoezi la kuwasajili wapiga kura wapya katika kaunti ya makueni amesema hatua yake kumtimua afisa mkuu mtendaji wa tume hiyo ezra chiloba imetokana na ukaguzi uliobaini kuwa pesa zilivujwa katika uchaguzi.