.
13th October, 2018
Muuguuzi mmoja wa kike anapigania maisha yake katika wadi ya wagonjwa mahututi baada ya kushambuliwa na mama anayedaiwa kughadhabishwa na taarifa za kufariki kwa mwanaye wa kiume mapema leo katika hospitali ya kitaifa ya kenyatta. Mama aliyetekeleza shambulizi hilo na anayedaiwa kuandamana na jamaa wengine watano hata hivyo ametiwa mbaroni huku shirikisho la wauguzi likitishia kuondoa huduma zao iwapo haki haitapatikana kwa mwenzao.