10th October, 2018
Watu hamsini na sita wameaga dunia kufikia jioni hii baada ya ajali ya barabarani kutokea katika eneo la Tunnel barabara ya Londiani kuelekea Muhoroni. Kwa mujibu wa mkuu wa polisi wa kaunti ya Kericho James Mugera, ajali hiyo ilitokea alfajiri baada ya basi la home boyz kubingirika mara kadhaa.