.
8th October, 2018
Serikali imepiga marufuku ya kuwatembelea watoto walio kwenye shule za mabweni, kuanzia sasa hadi mitihani ya KCPE na KCSE itakapokamilika. Akitangaza mikakati Iliyowekwa ili kudhibiti udanganyifu kwenye mitihani, waziri wa elimu Dr. Amina Mohamed pia amewaonya wazazi ambao watoto wao watapatikana na simu za rununu kuwa watawajibika wenyewe.