8th October, 2018
Uchaguzi mdogo wa nafasi ya useneta kaunti ya Migori ulifanywa leo ambapo vituo mbalimbali vya kupigia kura viliendesha shughuli hio kuanzia nyakati za asubuhi. Ingawa vituo vilifunguliwa kwa wakati, kulinakiliwa idadi ndogo ya wapiga kura waliojitokeza kushiriki zoezi hilo. Hivi sasa kinachoendelea ni hesabu ya kura katika vituo hivyo.