6th October, 2018
Tukiwa bado katika maswala ya kura ya maamuzi Seneta wa Baringo ambaye pia ni mwenyekiti wa chama cha KANU Gideon Moi amesema kuwa suala la kura ya maamuzi linatakiwa kuchukuliwa kwa uzito wala halitakiwi kupuuzwa na jamii ya wanasiasa katika taarifa kwa vyombo vya habari Gideon amesema kuwa wakenya wana haki ya kuichambua katiba na kupendekeza marekebisho kwa sababu wana sauti kubwa kuhusu utekelezaji wa katiba.
Gideon amesema kuwa wanasiasa wanatakiwa wayasikilize maoni ya watu kuhusu mabadiliko ya katiba wala si kuwakatia wananchi kauli.
Gideon ameongeza kuwa ni dhahiri wanachi wangependa katiba hiyo ifanyiwe marekebisho kwa sababu ya gharama ya maisha kupanda