2nd October, 2018
Katika kisa ambacho kimewaacha wakaazi wa Kijiji cha Chebior Kaunti ya Elgeyo Marakwet wakijiuliza maswali mengi, mwanamke mmoja ametoweka katika mazingira ya kutatanisha na hata kukosa kuhudhuria mazishi ya binti yake aliyeuawawa kinyama. Marehemu viterline jemutai ambaye aliuawa kwa kudungwa kisu mara kadhaa alikuwa mwanafunzi wa kidato cha 3 katika shule ya upili ya chebior. Sasa polisi wameanzisha msako wa kumtafuta mama ya marehemu huku wenyeji wakitafakari mikasa ambayo imeandama familia ya mwanamke huyo. Elvis kosgei na maelezo zaidi.