2nd October, 2018
Ni afueni kwa familia ya baba mmoja na wanawe wawili waliokuwa wakiishi ndani ya gari lililotelekezwa katika mtaa wa Kibera baada ya KTN kuangazia masaibu yao sasa wahisani wamejitokeza kuwasaidia. Hivi leo mke wa gavana wa Kaunti ya Nairobi Mike Sonko bi Primrose Mbuvi amewatembelea Ishmael Abdala khamis pamoja na wanawe wawili. Sasa ishmael ameaahidiwa kuwa atapata kazi katika kaunti ya nairobi huku bi mbuvi akiahidi kuwalipia karo ya shule wanawe wawili.