.
1st October, 2018
Wenyeji wa Elwak katika Kaunti ya Mandera bado wanalalamikia tukio ambako Maafisa wa Jeshi waliwapiga vibaya na kuwahangaisha baada ya gari lao kukanyaga bomu la kutegwa ardhini wiki iliyopita. Taarifa zinasema kuwa takriban mtu mmoja aliuawawa katika kisa hicho na kumi na saba kujeruhiwa. Gavana wa kaunti ya mandera ali robo alisema wiki iliyopita kuwa wanajeshi hao waliteketeza nyumba za wenyeji pamoja na kuua mifugo.