1st October, 2018
Malumbano ya kisiasa kati ya Naibu wa Rais William Ruto na kiongozi wa upinzani Raila Odinga yanaonekana kushika kasi baada ya wanasiasa wanaomuunga mkono Raila Odinga kujitokeza na kumjibu Ruto kuhusu shutuma zake alizotoa mwishoni mwa juma. Ruto alisema kuwa raila ana nia ya kumtimua katika chama cha jubilee kupitia salamu zake za heri na Rais Uhuru Kenyatta. Wakijibu shutuma hizo, mbunge wa Suna East Junet Mohammed na Gavana wa kaunti ya Mombasa Hassan Joho wamesema kuwa Ruto hata hafikii viwango vya Raila Odinga kisiasa.