27th September, 2018
Waakilishi wadi 32 katika kaunti ya Machakos sasa wanamtaka Gavana Alfred Mutua kuomba msamaha bila masharti kwa kumdhihaki spika wa bunge la kaunti hiyo.
Wakiongozwa na kiongozi wa wengi katika bunge hilo Mark Muendo waakilishihao wamemshutumu Mutua kwa kuwahujumu wakidai kuwa amekuwa akiwachochea wapiga kura dhidi yao. Zogo linahusu uteuzi wa mawaziri wa serikali ya kaunti ambapowaakilishi hao wamekuwa wakitilia shaka baadhi ya maamuzi ya Gavana Mutua.