24th September, 2018
Wanachama wa kamati mbali mbali za Bunge la Senati leo wamezuru mji wa Eldoret katika kaunti ya uasin ngishu kukadiria mafanikio na changamoto za utekelezaji wa serikali za kaunti. Maseneta hao wamefanya vikao vya bunge nje ya mji wa nairobi kwa mara ya kwanza katika hatua ambayo wanatarajia italeta mwamko mpya katika uongozi. Spika wa bunge hilo kenneth lusaka amesema kamati mbali mbali za bunge hilo zinafanya uchunguzi wa maswala mbali mbali ambayo yanaathiri wananchi ikiwemo sakata ya mahindi na kucheleweshwa kwa malipo ya wakulima.