.
23rd September, 2018
Bunge la Senate limemtaka Waziri wa Ugatuzi Eugene Wamalwa kufika mbele yake kutoa maelezo kuhusu ni kwa nini serikali imechelewesha malipo ya wakulima wa mahindi hata baada ya kuahidiwa kuwa wangelipwa.
Akizungumza baada ya kupokea maoni ya wakulima mjini Kitale Seneta wa Kaunti ya Uasin Gishu, Margaret Kamar, amesema ni dhuluma kwa wakulima kutolipwa baada ya kuwasilisha mazao yao katika halmashauri ya kitaifa ya nafaka na mazao NCPB.