.
18th September, 2018
Katibu mkuu wa muungano wafanyikazi nchini COTU Francis Atwoli leo hii amewataka waajiri wote watathmini upya mikataba ya makubaliano ya sasa ili waajiriwa waweze kustahimili hali ngumu ya kiuchumi inayoshuhudiwa nchini. Atwoli alikuwa akizungumza wakati wa kutia sahihi makubaliano mapya baina ya miungano ya wafanyikazi wa mashamba makubwa ambapo wafanyikazi walio kwenye muungano wa cotu pamoja na ule wa wakulima wa wapandaji watapata nyongeza kwenye mishahara yao kwa asilimia kumi na ishirini mtawalia.