.
15th September, 2018
Naibu wa Spika wa Nakuru Samuel Tonui na watu wengine kumi na mmoja wanazuiliwa katika kituo cha polisi cha Njoro kwa madai ya kuhusika kwenye vita vya kikabila katika maeneo ya Njoro kaunti ya Nakuru.
Watu tisa wameuawa na takriban kumi na watano kujeruhiwa vibaya.
Polisi na maafisa wa GSU wanaendelea kushika doria katika juhudi za kurejesha amani kati ya jamii zinazozozana.