.
1st September, 2018
Baadhi ya wazee kutoka Meru walikutana na Seneta wa Baringo Gideon Moi na kumuahidi kuwa watamuunga mkono kwenye kinyang'anyiro cha urais mwaka wa 2022. Wazee hao walioongozwa na professa albert mugambi na David Gituma walisema kwamba wameridhika kwamba moi atakuwa kiongozi bora kumrithi rais Uhuru Kenyatta. Walikutana naye huko ngata, kaunti ya Nakuru.