Wanajeshi watano wa KDF wauwawa kwenye msafara
29th August, 2018
Wanajeshi watano wa KDF wamefariki huku 10 wakiendelea kupokea matibabu, baada ya lori lao kukanyaga kilipuzi cha kutegegwa ardhini huko kiunga kaskazini mwa pwani ya kenya.
Shambulizi hilo lilitokea kwenye barabara kuu ya kuelekea Kiunga kutoka sehemu ya Sankuri mwendo wa saa mbili asubuhi.
Wanajeshi hao wa KDF walikua wakielekea vijiji vya kiunga katika msitu wa Boni kupeana misaada ya maji na vyakula kwa wakaazi hao.
Msemaji wa jeshi la KDF Paul Njuguna aliwashukuru wenyeji kwa ushirikiano wao baada ya tukio hilo.