28th August, 2018
Katibu mkuu wa muungano wa wafanyikazi wa serikali za kaunti, Roba Duba, amemkashifu Gavana wa Murang’a Mwangi wa Iria kwa kile anachodai kuvuruga usimamizi na uendeshaji wa shughuli za kusambaza maji katika kaunti hiyo. Duba amesema hatua ya gavana wa iria kuchukua usimamizi wa miradi yote ya maji chini ya serikali ya kaunti, ni kinyume cha sheria kwani hatua hiyo imewadhulumu wafanyikazi wengi kwa kuwaharibia ajira yao.