27th August, 2018
Shughuli ya usafiri kwenye barabara ya Nakuru kuelekea Nairobi ilitatizwa kwa muda katika eneo la five eight baada ya Mbunge wa Nakuru Town East David Gikaria akiwa na wafwasi wake kufunga barabara hiyo na kuyapaka rangi matuta.
Matuta hayo yaliyokosa alama yanasemekana kusababisha ajali kadhaa katika eneo hilo la barabara kuu. Gikaria pia anailaumu kenha kwa kutozingatia sheria maalum kama inavyofaa kwa kuikarabati barabara hiyo na hivyo kutishia kupeleka mswada bungeni utakayochunguza uwazi wa kenha inapokabidhi kandarasi za ujenzi wa barabara.