.
27th August, 2018
Magavana hii leo wamekongamana katika Kaunti ya Makueni kuangazia mfumo wa kuwahusisha wakaazi kwenye miradi yote ya maendeleo ili kuimarisha ugatuzi. Magavana 8 kati ya 47 walihudhuria mkutano huo unaotoa fursa kwa magavana kujifunza kwa kuangazia ufanisi na changamoto katika kila kaunti. Waziri wa ugatuzi eugene wamalwa wakati huo amesema changamoto kuu inayokumba ugatuzi ni jinamizi la ufisadi.