.
26th August, 2018
Gavana wa kaunti ya mombasa Hasan Joho, amewataka wakenya na viongozi kwa ujumla kushirikiana na serikali za kaunti ya ile ya kitaifakuhakikisha kwamba ardhi ya umma ambayo ilinyakuliwa miaka ya nyuma, imarejeshwa kwa serikali. Joho amesema kwamba serikali wakenya na viongozi wanafaa kuchukua hatua ya kuhakikisha kwamba wanalinda ardhi ya umma kwa manufaa ya vizazi vijavyo. Alikuwa akizungumza katika eneo la samburu.