23rd August, 2018
Naibu rais William Ruto amepuuzilia mbali matokeo ya kura ya maoni ambayo yamemworodhesha miongoni mwa viongozi fisadi akidai kuwa mani kama hayo ni msukumo kutoka kwa mahasimu wake wa siasa. Amesema kuwa hatayumbishwa na semi za wanaotaka kumchafulia jina akisisitiza kwamba kwa ushirikiano na rais Uhuru Kenyatta, atalenga darubini yake katika kufaulisha miradi ya maendeleo ili kuboresha maisha ya wakenya.
Akizungumza wakati wa mkutano na gavana wa Kirinyaga na wabunge 33 wa wadi kaunti hiyo, ruto amesema yuko tayari kwa ushindani na mahasimu wake wa kisiasa ila ushindani huu anasema sharti uwe katika misingi ya maendeleo.Wakati huo huo gavana waiguru amemhakikishia ruto kuwa eneo hilo zima liko nyuma yake na kwamba watamuunga mkono kisiasa.Waiguru pia amepuuza matokeo ya kura ya maoni ambayo pia yamemworodhesha.