.
22nd August, 2018
Shirikisho la riadha nchini limekashifu wanariadha ambao wanazidi kutumia dawa za kusisimua misuli huku wakisema kuwa kamati maalum itaundwa kupiga jeki vita dhidi ya utumizi huo.
Rais wa shirikisho hilo Jackson Tuwei amesema kuwa shirikisho la riadha halitasitisha vita hivyo, huku akigusia tu kwa umbali kuwa ni kero iwapo fedha ziltumika vibaya katika maandaliza ya ubingwa wa wanariadha wasiozidi miaka kumi na nane.