Wamemavyo Waganda:Wafuasi wa Bobi Wine wateta
20th August, 2018
Viongozi wa upinzani nchini Uganda wameshikilia kwamba
wabunge wa upinzani wamekamatwa, kunyanyaswa na kuzuiliwa na vyombo vya dola nchini humo.
Hii ni baada ya taarifa kusambaa kwenye mitandao ya kijamii,
ikionyesha mmoja wa wabunge hao akiwa katika hali
mbaya. Miongoni mwao ni Robert Kyagulanyi, mbunge na
msanii maarufu nchini humo kwa jina jingine Bobi Wine. Bobi
Wine amekuwa maarufu tangu kuingia bungeni mwaka
uliopita, na semi zake za kuushambulia uongozi wa rais
Yoweri Museveni zimepokelewa kwa shangwe muda wote na
wananchi waliochoshwa na uongozi wa serikali ya Museveni.
polisi nchini humo wanaarifu kwamba Bobi Wine na Francis
Zaake walikamatwa baada ya wafuasi wa mgombeaji mmoja
huru kurusha mawe kwa msafara wa rais Museveni,
siku ya juma tatu katika eneo la West Nile