14th August, 2018
Zaidi ya wabunge wa zamani kumi na watano kutoka eneo la Meru, wamefanya kikao na kinara wa upinzani Raila Odinga, na kuapa kuunga mkono juhudi za kuliunganisha taifa pamoja na vita dhidi ya ufisadi vinavyoendeshwa na rais Uhuru Kenyatta. Kundi hilo linalojiita Meru handshake forum, aidha limeunga mkono uhusiano baina ya rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga wakisema utachangia utangamano na uthabiti wa taifa.