8th August, 2018
Bingwa wa dunia mbio za mita 400 kuruka viunzi Nicholas Bett amefariki dunia wakati wa alfajiri eneo la Sochoi –Lessos kaunti ya Nandi .
Bett anaripotiwa kufariki papo hapo baada ya gari lake kuligonga tuta na kubingiria kwenye mteremko.Jamaa, marafiki na wanariadha walifika kuomboleza na familia katika hifadhi ya maiti kwenye hospitali ya Eldoret .