.
6th August, 2018
Kwenye kinyang'anyiro cha kiti cha useneta kaunti ya Migori, aliyekuwa mbunge wa Migori John Dache Pesa ametoa taarifa ya kuwa anaheshimu uamuzi wa chama cha ODM licha ya kwamba alikuwa anakimezea mate kiti hicho.
Chama cha ODM kilimkabidhi tiketi aliyekuwa mbunge wa Rongo zamani Ochillo Ayacko, hatua iliyompa mheshimiwa John Pesa uamuzi wa kuwaarifu wafuasi wake waliotaka agombee kiti hicho kuwa atawahudumia katika nyadhifa nyinginezo siku za usoni.
Amemshukufru kiongozi wa ODM Raila Odinga kwa kuendelea kutoa mwelekeo wa uongozi chamani. Kiti hicho kilibakli wazi baada ya aliyekuwa seneta marehemu Ben Oluoch Okello kuaga dunia.