5th August, 2018
Hali ya taharuki imetanda katika kijiji cha kapyego kaunti ya Elgeyo Marakwet baada ya wavamizi wanaoaminika kutoka kaunti jirani kuiba mifugo katika eneo hilo. Baadhi ya viongozi wamelalamikia utepetevu wa vikosi vya usalama unaolemaza jitihada za kupambana na wizi wa mifugo katika eneo hilo. Matukio ya hivi punde yanajiri baada ya eneo hilo kushuhudia mashambulizi ya mara kwa mara katika maeneo ya mpakani kati ya kaunti ya elegeyo marakwet, pokot magharibi na baringo.