2nd August, 2018
Jopo la wahariri limeikashifu hatua ya bunge la taifa kuwaagiza wanahabari wa gazeti la People Daily, wafike mbele ya kamati ya bunge la taifa ili kuelezea chanzo na uhalali wa habari iliyochapishwa kuwahusu wabunge.
Katibu mkuu wa chama cha wahariru, Christine Nguku, amesema hatua hiyo inakiuka haki za wanahabari. Lakini serikali kwa upande wake imesema ipo haja kwa wanahabari kuzingatia uwazi na usawa kwenye taarifa zao.